Monday, May 26, 2014

Misri: Al-Sisi hana uchu wa madaraka

Jeshi la Misri limekanusha ripoti za gazeti moja nchini Kuwait kuwa mkuu wa majeshi nchini Misri,Field Marshall, Abdel Fattah al-Sisi, atagombea urais.
Gazeti la al-Seeyassah, limemnukuu Field Marshall akisema kuwa hana budi ila kukubali wito wa wananchi wa Misri.
Field Marshall Al-Sisi

Lakini katika taarifa rasmi kupitia kwa mtandao wa kijamii, msemaji wake amesema kuwa ripoti hizo sio sawa na kuwa tangazo lolote la Al-Sisi kuwania urais atalitoa mbele ya wananchi wa Misri.
Field Marshall al-Sisi anaaminika kuwa nguvu au shinikizo la hatua ya jeshi la Misri kumuondoa mamlakani aliyekuwa Rais Mohammed Morsi.

No comments:

Post a Comment